Rapa Moni Centrozone amefunguka kwa mara nyingine tena na kudai hawezi kumuonea wivu Roma Mkatoliki kuhusiana na wimbo wake wa Zimbabwe ila wananchi ndiyo wanasababisha mpaka yeye aonekane anachuki na mwenzake.
Moni
ameeleza hayo baada ya majuma kadhaa kupita tokea atoe kauli yake mbele
ya kamera za eNewz ya EATV ambayo alidai hakufurahishwa na kitendo...
alichokifanya Roma kutoa wimbo wa Zimbabwe kwa kuita ni usaliti kwa kuwa
alijizungumzia yeye binafsi katika wimbo bila ya kuwashirikisha wenzake
ambao walitekwa pamoja.
"Hatuna mawasiliano mazuri
kati yetu kutokana na maneno ambayo yanaendelea katika jamii, mimi
siwezi kumuonea wivu Roma Mkatoliki kwa sababu yeye ameshafanikiwa
kimuziki tokea kitambo, nitawaonea wivu wakina Coyo pamoja na Billnass
ambao ndiyo kizazi changu kama endapo watafanya vitu vizuri na vikubwa
katika maendeleo yao lakini siyo kwa Roma", amesema Moni.
Pamoja na hayo, Moni amedai kitendo cha
yeye kuzungumzia wimbo wa Zimbabwe ndicho kinapelekea kuonekana kama
anachuki dhidi ya Roma.
"Mimi kuongelea zaidi mambo
ya Zimbabwe nimeoneka kama nina 'jelous' na kufanya watu waniongelee
vibaya 'so' imekuwa inaleta mtafuruku kwenye jamii, kiukweli
sijishughulishi na jambo lolote kuhusiana na Roma kwa sasa", amesisitiza Moni.
Pamoja na hayo, Moni amesema kwa sasa
anafanya kazi zake binafsi bila ya kumtegemea msaada wowote kutoka kwa
Roma kama ilivyokuwa awali hawajapatwa na tukio la utekwaji na watu
wasiojulikana.
0 comments:
Post a Comment