Monday, September 11, 2017
SLOANE STEPHENS ATWAA UBINGWA WA TENESI US OPEN
Mwanadada Sloane Stephens ameshinda ubingwa wa US Open 2017 baada ya kumfunga Mmarekani mwezake Madison Keys kwa seti 6-3,6-0 katika mchezo wa fainali, Sloane mwenye umri wa miaka 24, Imekuwa kama ndoto iliyotimia pasipo kutarajia baada ya miezi michache iliyopita alikuwa namba 83 katika viwango vya ubora wa Tenesi duniani.
Cha kushangaza kutoka kwa mwanadada huyo ni amerejea uwanjani baada ya kufanyiwa upasuaji wa...
mguu wake miezi 6 iliyopita hata hivyo Sloane na mcheza tenisi mwenzie Madison Keys mwenye umri wa miaka 22 ni marafiki wa kutupwa na hii ilikuwa ni fainali yao ya kwanza ya Grand Slam.
.
Kizuri zaidi ni kwamba Baada ya mechi wawili hao ambao ni marafiki wa karibu zaidi tangu utotoni,wamekumbatiana na kupongezana huku familia ya mwanadada sloane ikiwa uwanjani kushuhudia fainali hiyo.
.
Labels:
HABARI & UDAKU
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment