Pages

Subscribe:

Monday, September 11, 2017

AMBER LULU: NIMEWEKEZA PESA KWENYE KAZI LAZIMA NIWE MAKINI

Msanii wa muziki wa kizazi kipya aliyejipatia umaarufu kwa kupiga picha za utupu, Amber Lulu amesema sasa hivi ana 'stress' za kazi zake hivyo hataki kuyapa nafasi mambo ambayo yatamuharibia. 

Akizungumza na mwandishi Amber Lulu amesema sasa hivi hataki mambo ya skendo ikiwemo kujibizana na 'video queen' mwenye...
sifa kama yake Amber Ruth, pamoja na picha za utupu ambazo ndiyo zilimpa umaarufu.

"Hivyo vitu siwezi kuviendekeza tena sasa hivi, nina 'stres' za kazi zangu. Nimetia pesa kwenye kazi sasa lazima niwe makini na masuala ya msingi", amesema Maber Lulu.

Amber Lulu hivi sasa ameamua kufanya muziki ambapo mpaka muda huu ana kazi mbili sokoni, ikiwemo 'watakoma' na 'Give it to me'.

0 comments:

Post a Comment