Pages

Subscribe:

Saturday, September 9, 2017

MBOTO: SIMBA KATWAA NGAO YA HISANI YANGA ATATWAA UBINGWA

Muigizaji wa filamu bongo, Haji Mboto ambaye ni shabiki wa Yanga amewapiga vijembe watani wao wa jadi klabu ya Simba kuwa licha ya kuanza kwa kishindo Ligi Kuu Bara kwa kuwanyuka Ruvu Shooting bao 7-0 bado  uhakika ubingwa utaelekea jangwani. 

Mboto ambaye mara kwa mara amekua akionekana kuikejeli Simba katika mitandao ya kijamii amesema wao ndiyo mabingwa wa kihistoria wa ligi na hata...
wakianza kwa kutoa sare huwa wanamaliza ligi kwa ubingwa kama walivyofanya msimu uliopita.

Amesema kwamba msimu uliopita Azam Fc walitwaa Ngao ya Jamii lakini mwishoni mwa msimu Yanga ikatwaa ubingwa,lakini msimu huu Simba wametwaa Ngao ya Jamii vivyo hivyo lazima ubingwa utatua kwao ukiwa ni wa msimu wa nne mfululizo.

Aidha ameenda mbali zaidi kwa kusema kwamba wao kama Yanga hawataki kuwa kama Rais wa Burundi Piere Nkurunziza hivyo pindi watakapotwaa ubingwa msimu huu watakaa chini na wanachama wenzao ili kuamua kuwaachia wapinzani wao ili wapate nafuu ya kuchekwa mitaani.

Yanga ambao ni mabingwa watetezi wa VPL walianza kwa sare ya kufungana bao 1-1 na Lipuli FC ya mkoani Iringa huku Simba ikiiunguruma kwa ushindi wa jumla ya bao 7-0 dhidi ya Ruvu Shooting na sasa inaongoza katika msimamo wa ligi kuu soka Tanzania Bara.

0 comments:

Post a Comment