Pages

Subscribe:

Tuesday, November 1, 2016

GOODLUCK GOZBERT: MOYO MASHINE SIYO WIMBO WA BONGO FLAVA


Mkali alie iandika ‘Moyo mashine’ ya Ben pol amesema ajawahi kukaa kuandika nyimbo za bongo fleva licha ya kuziandika ngoma nyingi zilizo fanya vizuri katika soko la Bongo fleva. Goodluck Gozbert maarufu kama (lolpop) ambaye ni muandisi wa ala za muziki na muandishi wa mashairi pasi kusahau ni nyota wa kuimba mziki wa injili. 

Akipiga story, Goodluck alisema kuwa yeye yupo kwa ajili ya kumtumikia Mungu na kuinua mioyo iliovunjika, hivyo ajawai pendezwa kuitwa...
muandishi wa bongo fleva, yeye uandika mashairi ya kuelimisha tu, tafsiri inayozaliwa kuwa nimuandishi wa bongo fleva nikile anacho andika kina imbwa na wanamuziki wa Bongo fleva.
 
”kunamashairi mengi uimbwa na wanamuziki wa gospel yangeimbwa na mtu wa bongo fleva tungesema bongo fleva na kinyume yake ni hivyo hivyo”. alisisitiza Goodluck.

goodluckgozbert-20161031-0002
Goodluck amesema afanyi biashara yakuandikia watu ngoma za bongo fleva, ngoma alizo ziandika kwa Mo-music, Baraka the Prince, Ben Pol nimazingira ya wao tu kama marafiki yaliteleza kuzalisha kitu, kwa hiyo yeye hawa watu kwake sio kama wasanii wa bongo fleva bali ni marafiki
wakaribu.
Amemaliza nakusema ajawahi kufuatilia
maendeleo ya hizo ngoma alizo andika,
akishamkabidhi mtu basi imeishia hapo, yeye uendelea na harakati zake za kumtumikia Mungu wake kwani ndio wito wake alio nao moyoni mwake.

0 comments:

Post a Comment