Pages

Subscribe:

Wednesday, August 16, 2017

BAADA YA KUTOA NYIMBO MBILI KWA MPIGO SASA DARASSA KUJA NA HII NYINGINE

Ikiwa miezi mitatu imepita tangu Darassa kuachia ngoma yake mpya 'Hasara Roho' ambayo kwa nafasi yake imeweza kufanya poa na kuwafikia watu wengi zaidi ingawa haikuweza kufikia matakwa ya baadhi ya watu ambao walionekana wakidai ni wimbo wa kawaida.

Darassa ametangaza kuachia kazi yake mpya ndani ya mwezi huu wa nane ambayo kwa mujibu wa kile alichoanza kuweka kwenye mitandao ya jamii huenda kazi hiyo ikaitwa...
'Hakuna Wasiwasi".

Darassa mwishoni mwa mwaka jana aliachia wimbo wake 'Muziki' ni wimbo ambao ulileta mapinduzi makubwa katika muziki wa Bongo fleva hususani kwa wasanii wa Hip hop kwani uliweza kuwa wimbo maarufu zaidi kwa muda mrefu, huku ukichezwa kila kona na kuimbwa na kila rika ndani ya nchi hata nje ya nchi.

Muziki ni video ya kwanza kwa wasanii wa Hip hop Bongo ambayo mpaka sasa imetazamwa na watu wengi kwenye mtandao wa You Tube kwani imefikisha watazamaji zaidi ya milioni tisa.

0 comments:

Post a Comment