Tuesday, September 12, 2017
ALBAMU YA DR DRE NA EMINEM KUJA KUFANYA MAPINDUZI YA MUZIKI NCHINI MAREKANI
Baada ya baadhi ya Albam kutikisa hivi karibuni ikiwemo albam ya Grateful,Damn,More life sasa wewe mpenzi wa muziki kutoka mbele tegemea ujio mpya kabisa kutoka kwa wakongwe wawili ambao mapka kufikia leo inasemekana wamesha kamilisha ngoma za kutosha ili waje kufanya mapinduzi katika muziki na kuonyesha kuwa wao ni wakongwe.
Mapinduzi hayo yanaletwa na mkali wa midundo kutoka Marekani Dr Dre na rapper Eminem baada ya hivi karibuni kuthibitisha kuwa...
wapo jikoni wakiandaa Albam yao mpya ambayo itakuja kufanya mapinduzi ya Albam zote zilizotoka mwaka huu,Kwamujibu wa The Defiant Ones director, Allan Hughes amesema “Dr Dre bado anarekodi na watu awajui hili kuwa bado mkali Dre bado anafanya kazi yake ya kuandaa muziki kama kawaida” Amesema Dre nikama Picasso ambaye anapaka rangi kila siku.
Labels:
HABARI & UDAKU
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment