Mwanamuziki anayesumbua kwa sasa na ngoma ya 'Tunafanana' Barnaba Elias
'Barnaba Classic' ametupa jiwe gizani linalodaiwa kuwa ni dongo kwa
mzazi mwenzake baada ya kufunguka kwenye mtandao kuwa kumtukana mwanamke
ni sawa na kumtukana mzazi wake.
Dongo
hilo Barnaba ameliweka kwenye ukurasa wake wa Instagram baada ya mzazi
mwenzake huyo kudai kuwa baada ya miaka mtano kupita hatimaye sasa
amefanikiwa kupata...
amani ya moyo ambayo ndicho kitu alichokuwa akikikosa
kwa muda wote.
Barnaba ameandika "Mama
aliniambia ukimtukana mwanamke basi umenitukana na mimi. Siku zote
nawaona kama mama zangu hongera wanawake wote duniani Salamu zangu juu
yenu Jumapili ya leo nawapenda Sana"
Ujumbe wa Barnaba aliouweka Instagram jana baada ya ujumbe wa Mzazi mwenzake Mzazi mwenzake Barnaba, Zuu Namela ambaye walibahatika kupata mtoto wa kiume 'Steve' jana asubuhi aliandika kwenye ukurasa wake wa Instagram kisha kufuta ujumbe huu.
"Ni watu wachache sana wanaojua nikitu gani nilikua nakosa katika maisha yangu! Unaweza ukapata kila kitu kwenye maisha ila ukakosa furaha,amani,heshima......kwa zaidi ya miaka mitano hichi ndo nilicho kuwa nakitafuta #AMANIYAMOYO "
Ujumbe wa mzazi mwenzake Barnaba, Bi Zuu Namela kabla ya kuufuta.



Follow on Instagram
0 comments:
Post a Comment