Pages

Subscribe:

Tuesday, March 14, 2017

CR7 KUANDAA NYUMBA YA BIL13 KWA WATOTO ZAKE MAPACHA WATAKAO ZALIWA

Cristiano Ronaldo Georgina Rodriguez
Mwanamitindo maarufu nchini Hispania, Georgina Rodriquez ambaye ni mchumba wa mshambuliaji wa Real Madrid na timu ya Taifa ya Ureno, Cristiano Ronaldo, anatarajia kujifungua watoto mapacha.

Kwa mujibu wa Gazeti la The Sun limeripoti kuwa, mchezaji huyo ameweka wazi kwamba ameandaa nyumba yenye thamani ya Sh bilioni 13 kwa ajili ya kufikia watoto hao na pia ameweka...
vito mbalimbali vya thamani kwa ajili yao.

Ronaldo ambaye kwa sasa ana mtoto mmoja wa kiume anayejulikana kwa jina la Cristiano Jr, ujio wa watoto hao utaongeza ukubwa wa familia yake lakini kwa mchumba wake huyo mwenye umri wa miaka 23 itakuwa ndio watoto wake wa kwanza.

Kupitia akaunti ya Instagram, Georgina amedai kuwa familia hiyo kwa sasa ipo katika furaha kubwa ikiwa inatarajia kupata watoto hao wawili. “Muda mfupi ujao familia itakuwa kubwa na Cristiano Jr. anatarajia wadogo zake wawili, tuna furaha mno,” aliandika Georgina.

0 comments:

Post a Comment