Mwanadada anayetamba na ngoma ya Main
Chick, Maua Sama amesema yeye hategemei ‘kiki’ ili ku-‘hit’ bali uzuri
wa kazi zake, na kuwataka wasanii wengine waache kutafuta ‘kiki’ ili
kupata majina bali wajikite kwenye kutengeza kazi nzuri.
Akiwa ndani ya Planet Bongo jana, Maua
amesema kuwa wasanii wengi wamejikita kwenye kutafuta kiki badala ya
kuwapa mashabiki ladha tofauti na kusisitiza kwamba dhana ya kiki
inapaswa...
kufutika ili kila mtu afanye kazi nzuri.
“Ukifanya muziki mzuri lazima tu
utapata jina, wala hakuna haja ya kiki, mfano mzuri mimi hapa ni msanii
ambaye nimepata sapoti nzuri sana kwenye ‘game’ bila kuongelewa kwa
mambo mabaya ya kiki, ‘The real deal is good music’ siyo skendo, japo
mimi nina skendo ya kutoa ngoma kali siku zote”. Alisema Maua ndani ya kipindi hicho.
Sama ameongeza kwamba katika muziki wapo
wasanii ambao wanafanya muziki mbaya lakini wanapewa nafasi kubwa ya
kusikilizwa kutokana na kiki lakini hana chuki nao kwani pia watu wa
aina hiyo wana mashabiki zao wanaopenda kuwasikiliza.
“Mimi nina wivu wa maendeleo
sana, lakini sina chuki na watu wanaofanya muziki mbaya kwani hata wao
wana masoko yao na wanauza ila kinachotokea kwangu nikimuona mtu katoa
kazi mbaya mimi naingia kutengeneza ‘hits’ kali ili nipate soko zaidi”. aliongeza Maua.
Hata hivyo Maua ameongeza kuwa msanii
yoyote ambaye huandika nyimbo zake kipindi anapokuwa kwenye hisia yoyote
ni wazi wimbo huo ukiachiwa hewani lazima uwe mkali kwa kuwa unakuwa
umebeba uhalisia na hisia za kweli.



Follow on Instagram
0 comments:
Post a Comment