Pages

Subscribe:

Thursday, March 16, 2017

PROF JAY: SITOIMBA TENA MUZIKI WA SINGELI

Mkongwe wa bongo fleva  kwenye mahadhi ya hip hop, Prof Jay wa Mitulinga jana amedropisha ngoma yake  mpya inayokwenda kwa jina la ‘Kibabe‘ ambao ni hiphop iliyozoeleka kutoka kwake  baada ya kukaa mda mrefu tangu atoe wimbo wenye mahadhi ya hip hop singeli ulioitwa ‘Kazi kazi’

Prof. Jay ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mikumi amesema nyimbo za kiharakati zilimpelekea kuwa Mbunge kabla ya kuingia Bungeni kwa kuwa kila wimbo ambao aliokuwa anaufanya ulikuwa unabeba...
shida za wananchi kiuhalisia na kuendelea kusema kuwa hawezi kubadilika.

Mbali na hilo Prof Jay amewataka wasanii wa singeli kukomaa katika muziki huo  ili waweze kuufikisha mbali na siyo kubweteka kusubiri watu wengine kuwanyanyua ili waonekane. Alidai  yeye hana mpango wa kuendelea kuimba muziki huo na kwamba alijitoa kufanya  wimbo mmoja ili kuonesha vipaji vilivyopo kwenye muziki huo ikiwa ni pamoja na  kuupa hadhi kwenye jamii.

“Mimi napenda kusapoti vipaji vilivyopo mitaani,  hata leo ukinipa jezi nicheze mpira ili kuhamasisha watu waupende mpira nitacheza lakini siyo sehemu yangu, kuhusu Singeli mimi siwezi tena kuimba nilivyoimba ule wimbo nilitaka kuonesha jamii kuwa kuna muziki huu pia upeni ushirikiano, sasa wasanii wenye wimbo huo ndiyo wenye jukumu la kuhakikisha unakua, Mwaka huu wameonekana kupooza wanatakiwa wapambane” Jay alisisitiza ndani ya Planet Bongo.

0 comments:

Post a Comment