Pages

Subscribe:

Friday, March 10, 2017

AIKA: VANESSA NDIYE ALIYE TUFANYA TURUDI KWENYE MUZIKI



Muimbaji wa kundi la Navy Kenzo, Aika, amedai kuwa Vanessa Mdee ndiye aliyewahamasisha kurudi kwenye muziki baada ya kuwa wamekata tamaa.Akizungumza jana kwenye kipindi cha Ngaz Kwa Ngaz cha EATV ambapo yeye na Nahreel walikuwa ma-hosts, Aika amemuelezea Vee Money kama mtu mwenye upendo.

“Ni msichana ambaye ana bidii, ametumotivate vitu vingi sana hata sisi kwenye maisha yetu,” amesema Aika. “Tuseme, yeye ndiye alitufanya sisi turudi kwenye muziki baada ya...
kuja studio na kusikiliza nyimbo zetu na kusema ‘jamani toeni hii nyimbo ya Bokodo’ by then. Alitupa nguvu sana na ni mtu ambaye amekuwa akituencourage tukisaidiana,” ameongeza.

Vee Money pia aliwahi kuzungumzia story hii.
Akizungumza kwenye kipindi cha Up Close & Personal cha K24 ya Kenya, Vee alisema alikutana na Nahree na Aika baada ya kupigwa chini na label ya B’Hits.

“Kwahiyo nikasema nahitaji kumpata mtu ambaye anaweza kupatia sauti yangu. Shout out kwa Hermy kwasababu sasa sisi ni familia, ni kaka yangu daima. Kwahiyo nilikuwa naijua hii bendi ya Navy Kenzo toka Arusha na wakati huo walikuwa wakijulikana kama Pah One. Pah One ikaja kuvunjika na wawili kati yao walikuwa wanataka kwenda nje kusoma masters, nilienda kwenye studio yao ambayo wakati huo ilikuwa nyumba yao na nikamuambia Nahreel ‘nakuaminia, nadhani mimi na wewe tunaweza kufanya mambo makubwa pamoja,’” alisema Vanesa.
“Muda huu Nahreel alikuwa tayari kufungasha virago na kuondoka ‘nimechoka na mambo haya ya muziki.’ Na nikamuambia, acha tufanye kazi na nikamuambia ‘nichezee nyimbo zako’ pamoja tulielewana sana na imekuwa ni story tangu hapo na ninajivunia sana Navy Kenzo na Nahreel ni genius na ndiye mtayarishaji mkuu wa album yangu.”

0 comments:

Post a Comment