Msanii wa muziki na mwalimu wa dance,
Msami Giovani anayefanya vizuri na wimbo wake wa “So Fine”, akiwa
amemshirikisha rapper wakike anaye fanya vizuri, Chemical. Msami Baby
ameweka wazi hisia za moyo wake na kusema kuna mastaa wa ‘bongo movie’
anatamani kutoka nao kimapenzi.
kushindwa kuchagua mmoja kwa kuwa wote ni wazuri.
“Katika Mastaa wa Bongo ambao
ninawapenda sana na natamani ningewapata ni pamoja na jokate mwegelo,
Elizabeth ‘Lulu’ Michael Pamoja na Wema Sepetu, Nawapenda sana hao
wadada na ni wazuri Sana” Alisema Msami kwenye kipindi cha Pillow Talk cha Timesfm.
Kwa upande mwingine msanii huyo amesema
yeye umri kwake siyo kigezo kikubwa kwakuwa ameshawahi kutoka na
mwanamke aliyemzidi umri na wakaishi vizuri bila ya kuwa migogoro ya
aina yeyote ile.
0 comments:
Post a Comment