Pages

Subscribe:

Tuesday, May 29, 2018

WEMA AKOSEKANA MAHAKAMANI BAADA YA KWENDA INDIA KUFANYIWA UPASUAJI

Msanii Wema Sepetu anayekabiliwa na kesi ya kutumia dawa za kulevya ameshindwa kufika katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo May 29, 2018 ili kujitetea katika kesi yake kwa sababu amekwenda nchini India kufanyiwa upasuaji.

Hayo yameelezwa na Mama mzazi wa Wema, Mariam Sepetu mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba baada ya Wakili wa serikali, Constantine Kakula kuhoji kwanini...
Wema hakufika mahakamani.

Wakili Kakula amedai kuwa anashangaa kutokumuona Wema, kwani hata ahirisho la mwisho la kesi yake hakuwepo.

Baada ha kueleza hayo, Mama Wema akatoa nyaraka za Wema za kusafiria na kuieleza mahakama kuwa Wema anaumwa na amekwenda nchini India kufanyiwa upasuaji.

Wakili Kakula amedai kuwa hakuna uthibitisho wowote wa kuonyesha Wema anaumwa, hivyo anaiomba mahakama isimamie sheria.

Kutokana na hoja hiyo, Hakimu Simba amesema ni kweli hakuna uthibitisho, hivyo katika tarehe ijayo uthibitisho unapaswa kuwepo, ambapo ameahirisha kesi hiyo hadi June 13,2018.

Mbali na Wema, washtakiwa wengine ni Angelina Msigwa na Matrida Abbas. 
Kwa pamoja wanakabiliwa na mashtaka mawili ya kukutwa na kiwango kidogo cha dawa za kulevya na kuzitumia.

Inadaiwa Februari 4, 2017 katika makazi ya Wema eneo la Kunduchi Ununio, washtakiwa walikutwa na msokoto mmoja na vipisi vya bangi vyenye uzito wa gramu 1.08.
 
Kwa upande wa Wema yeye anadaiwa kuwa February mosi 2017 katika eneo lisilojulikana jijini Dar es Salaam, alitumia dawa za kulevya aina ya bangi.

0 comments:

Post a Comment