Pages

Subscribe:

Friday, May 26, 2017

KAULI YA DIAMOND SIKU MBILI KABLA YA KIFO CHA IVAN

Mwimbaji Diamond Platnumz alikaa kwenye Exclusive Interview na On AiR with Millard Ayo siku mbili zilizopita na kuzungumzia ishu mbalimbali akiwa na kundi lake la WCB kwenye kumtambulisha msanii mpya wa WCB aitwae Lavalava.

Pamoja na maswali mengine, Diamond alijibu kuhusu Mpenzi wake Zari kwenda kumjulia hali Ivan ambaye ni mzazi mwenzie ambapo japo Mashabiki wengine walionyesha kutopenda Zari kumjulia hali, Diamond alisema... hana neno kabisa na Zari kwenda kumjulia hali sababu hata kama waliachana yule atabaki kuwa ni mzazi mwenzie na alifanya vizuri kwenda.

Kwenye hii video hapa chini maswali mengine Diamond aliyoyatolea majibu ni iwapo angekua South Afrika, angekwenda Hospitali kumjulia hali Ivan? ……………….R.I.P kwa Ivan ambaye amefariki alfajiri ya kuamkia May 23.

0 comments:

Post a Comment