Pages

Subscribe:

Monday, July 31, 2017

DIVA THE BAWSE: MIMI SIYO TEAM KIBA NA SIHITAKI HATA KUSIKIA


Alhamisi ya wiki iliyopita kwenye kipindi cha Ala za Roho cha Clouds fm Diva The Bawse (Mtangazaji) alikuwa na interview na Wachekeshaji wapya wanaokiki mjini kutoka kampuni ya Timamu Ebitoke na Mama Ashura.

Moja kati ya story ambazo zilikiki kinoma kwenye interview hiyo ni story za u-team kwenye game ya Bongo fleva ikiwa siku chache zilizopita alisikika Mama Ashura akifunguka kuwa yeye ni shabiki mkubwa wa Diamond Platnumz na sio Alikiba, huku Ebitoke yeye ni shabiki wa kutupwa wa...
Alikiba.

Kwenye interview hiyo Mama Ashura alionekana kuibuka kidedea kutokana na uwezo wake wa kuongea kumzidi Ebitoke na vitu kama hivyo, huku akisimama kwenye point ya kumshauri Alikiba atoe ngoma mpya ili aweze kurudi kwenye soko la ushindani wa muziki na wasanii wengine kama Diamond Platnumz ambaye amedropisha ngoma mpya 3 kwa mkupuo.

Wapo ambao waliomjia juu Mtangazaji Diva The Bawse kwa kumkaribisha mtu kama Mama Ashura kwenye interview hiyo ikiwa hapo awali walikuwa na dhana kuwa huenda Diva akawa ni Team Kiba kutokana na alivyozoeleka kuelezea hisia zake juu ya msanii Alikiba.

Diva amewapa makavu yao watu hao kwa kuandika waraka mrefu kwenye ukurasa wake wa instagram na kuelezea the way ambavyo anahitaji kusalia kwenye taaluma yake ya utangazaji na uana habari na hivyo hana team hata moja ambayo anaishabikia.

Kupitia page yake hiyo Diva ameandika kuwa:

 “Nimepata malalamiko baadhi ya watu Oh Kwann umemualika @mamaa_ashura wewe si team Kiba Oh Diva this and that,
Naomba ni make it very clear mimi sina U team, mambo ya Uteam yanagawa mashabiki wangu , sitaki kwanza ata kusikia mambo hayo tena, Im over that Path … Mungu mwenyewe anajua nilivyo busy saa Hii bulding my life and my future Jaman , hv alot in my plate sahan yangu imejaa sana , huo muda tena sina tena n lov erybody yes napenda kila mtu ata haters sababu wananifanya niwe famous n idgaf yes ila sichagui sibagui ataenizika simjui wanasema waswahili, Mi nahudumia watu wote sihudumii pande1 tu, Sitak Gawa shabiki zangu sababu ya vitu ambavyo havinipi faida maishani, tuendeleen kuwa marafiki tuheshimiane , hivyo basi namualika yoyote kwenye show yangu nikijisikia na watu wakimuhitaji, sina Pande yoyote ile Niko busy nafanya kazi yangu na naiheshimu sana Kama ninavyoiheshimu serikali , nawapenda sana ila being Profesheno kumenipenda Zaidi, I chuz to be happy and means i’ll support good music regardless, na ukinikosea Ima free shot you with Nothing but the truth, Ima freesoul
peace out!!
Mbarikiwe na Bwana!!”

0 comments:

Post a Comment