Pages

Subscribe:

Friday, April 27, 2018

AKOTHEE ATAMANI KUONGEZA MTOTO WA SITA


MSANII mwenye vituko kutoka nchini Kenya, Esther Akothee, kidizaini kama anatamani kuongeza mtoto wa sita baada ya kuacha meseji tata mtandaoni. Mkali huyo wa Ngoma ya Oyoyo ambaye haishi vituko kila kukicha, juzikati aliwapa sapraiz mashabiki wake kwa kusema kuwa endapo atabeba mimba tena, basi lazima kuwe na mkataba.

“Mhmmm vile wanaume walinizalisha na kuniacha hoi! Wakati huu nikibeba mimba ni mpaka contract (mkataba)! Kwanza tuweke account ya mimba! iiitwe...
pregnant account (akaunti ya mimba), post natal account (akaunti ya kujifungua), school fee account (akaunti ya ada ya shule) na holiday account (akaunti ya mapumziko).
Bila hizi Sheria kutimizwa! Nenda uzae nje au ununue mtoto! Hamtujazi ujinga. Angalia fridge pale nyuma! Sasa nikule watoto ama? Na ndiyo nimetoka hospitali na mtoto mgeni.

Baba na lawyer wako wapi?” Aliandika Akothee katika ukurasa wake wa Instagram na kuweka picha akiwa na baadhi ya watoto wake. Akothee mwenye watoto watano, kwa sasa yupo katika uhusiano na meneja wake, Nelly Oaks.

0 comments:

Post a Comment