Pages

Subscribe:

Tuesday, September 6, 2016

RAYMOND AONGEA HAYA BAADA YA KUMPANDISHA AVRIL KWENYE JUKWAA

Raymond alisababisha yowe kubwa mwishoni mwa wiki katika show ya WCB mjini Mombasa alipompandisha mrembo wa Kenya, Avril aliyekuwa mmoja wa watu waliohudhuria.

Raymond amefunguka;
Sikutegemea kabisa kwamba nitamuona Avril katika show , walikuja watu wengi lakini wakati nipo stejini nikaona VIP kama kuna mtu kakaa, kuangalia vizuri nikaona ni Avril so kwa heshima yake na thamani ya muziki wake nikaona...
kaja kwenye show ambayo naperform nikaona kabisa ni heshima kubwa kaonesha, nisingeweza kuonesha tu kwa kutaja jina lake kwa mbali, nikatamani aje stejini, nikatamani niwe naye stejini. Namshukuru kaja kwenye show na sikutegemea kumuona. 

Ndio nikamuita kwenye steji nikamuimbia watu wakafurahi, naye amefurahi naye mwenyewe alifurahi, na kuonesha kuwa alifurahi pia, kapost hadi picha tukiwa stejini naye amesema ameappreciate. 

Kikubwa nilichokigundua pale ni support kutoka moyoni kabisa, sababu ukiangalia Avril ni msanii wa nchi nyingine kabisa na mimi ni msanii wa nchi nyingine, lakini katoa dhana ya matabaka, kavuka boundaries, kaonesha kuwa sisi ni ndugu tunasapotiana. Kiukweli nimefurahi sana na naamini na yeye kafurahi.

0 comments:

Post a Comment