Pages

Subscribe:

Thursday, September 15, 2016

DADA WA DIAMOND PLATNUMZ AKIRI KUPENDA PETIT MAN

Dada wa Diamond ameamua kufunguka ya moyoni na kudai anampenda sana mume wake Petit Man ambae walitengana kwa muda kutokana na kutokuelewa hapa na pale lakini kwa sasa inaonekana wameweka mambo sawa. Ameandika haya kwenye ukurasa wake

_esmaplatnumz
Baby dady mkimuona mwambieni mi Nampenda tuu ukiniuliza hata sijui... kuna wakati unaweza kufichaficha au kujionesha hupendi au ukajikaza usiseme unachojisikia kusema but mi naona bora... uwe muwazi ili roho yako Iwe na Amani... Jamani mi Nampenda huyu kaka plz nyakunyaku kuweni makini huyu mi nahisi km kafika kigoma mwisho wa reli...na natania msije nikomoa...hamchelewi...

0 comments:

Post a Comment