Pages

Subscribe:

Sunday, May 10, 2015

WEMA: RAY NA STEVE NYERERE WANAFIKI WAKUBWA


Wema: Ray, Steve Nyerere Wanafiki Wakubwa
Staa wa Bongo Movies, Wema Sepetu ‘Madam’ juzikati alijikuta akivunja ukimya kwa kusema kwamba, wasanii wenzake Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ na Vincent Kigosi ‘Ray’ ni wanafiki wakubwa baada ya kumtosa kwenye Pati ya Instagram iliyofanyika hivi karibuni jijini Mwanza.
Akizungumza na paparazi, Wema alisema alikubaliana na mastaa hao kutoenda kwenye Shoo ya Zari All White Party iliyofanyika Mlimani City jijini Dar badala yake...
waongozane naye jijini Mwanza lakini wakamgeuka.
“Sitaki kabisa nisikie mtu ananiambia habari ya Steve Nyerere au Ray maana ni wanafiki wakubwa, hawawezi kuniahidi kutokwenda pati ya Zari lakini wakaenda na wasije Mwanza kama walivyoniahidi,” alisema Wema.Paparazi wetu baada ya kupata malalamiko ya Wema, alimsaka Steve ili aweze kuzungumzia unafiki wao, akafunguka:
“Kweli mimi na Ray tuliahidi kuungana na Wema kwenye shoo yake ya Mwanza ila siku ya mwisho tulikwama baada ya kupungukiwa fedha ya nauli, hivyo tukashindwa kabisa na tusingeweza sisi kwenda huko kwa kumtegemea yeye atulipie kila kitu.Tukaona twende kwa Diamond ambaye naye alitualika.

0 comments:

Post a Comment