Pages

Subscribe:

Wednesday, May 27, 2015

WAUZA SURA WAMCHANGANYA BATULI

Staa wa Bongo Movies, Yobnesh Yussuf ‘Batuli’ amekiri kuteswa na suru nzuri za wanaume ambao huwa wanamfuata kwa ajili ya uhusiano wa kimapenzi huku wengine wakimuahidi kumuoa na kuwakubalia ombi lao na kuelekeza mapenzi yake yote kwao.
Azungumza na tanuru la fulamu hivi karibuni  batuli alisema kuwa yeye huwa anapenda mwanaume mpole na mwenye... kujiheshimu ili watengeneze maisha yao na penzi linapo kolea na kujiachia kimahaba sura hizo hubadilika na kuwa mwiba kwake hali ambayo humfanya  akimbie.

“Nina watoto wawili  ambao nimezaa na wanaume wawili tofauti, niliwahi kuolewa na mwanaume aliekuja na lugha nzuri na sura yenye  kuonyesha  ana mapenzi ya dhati lakini baada ya kuingia ndani ya ndoa akakunjua makucha nikaamua  kukimbia  vivyo hivyo  na wapili nilimpata kwa staili hiyo naye akawa mchungu” alisema Batuli.

Staa huyo alisema kwamba kwasasa ana mchumba ambaye badoanamwangalia kama naye ni kama aliowahi kuwakubali na  na kuingia nao kwenye ndoa kasha wakawa mbogo ndiao mana ameweka ngumu kuolewa sasa mpaka ajue tabia yake kwani amechoka kuumizwa na wanaume.

0 comments:

Post a Comment