Pages

Subscribe:

Friday, May 8, 2015

ANDIKO LA WEMA KUHUSU SHERIA YA MAKOSA YA MTANDAO LAUNGWA MKONO

Naomba mimi kama Wema Sepetu, nitoe tamko langu rasmi kuhusu hii Sheria mpya iliyopitishwa bungeni. Naongelea Sheria ya cybercrime au cyberbulling. Ukweli ni Kwamba watanzania tunatumia vibaya mitandao ya kijamii. Matusi yamekuwa ni mengi na sometimes hawavumiliki. Kwa kweli kunahitahija Kuwa na... laws in place za kupunguza unyanyasaji kupititia mitandao ya kijamii. That said, yes nai support hii bill ya cyber crime to an extend.

Kama jinsi ambavyo watanzania tunatumia vibaya mitandao kwa kuumizana kwa njia ya matusi na kuchafuana, wana siasa wetu waliopitisha hii Sheria ya cybercrime pia wameitumia vibaya hii Sheria na kuitumia kama silaha ya kumfunga mdomo mtanzania.

Kusema ukweli mimi kama Wema Sepetu nimechoka kutukanwa, mpaka mama yangu mzazi anadhalilishwa humu Kwenye mitandao. Kuna kipindi nilifikia hatua ya kuwaza bora nife tu ili kuepukana na matusi na kuandikwa na magazeti kwa habari za uongo.

 Lakini as much as ningependa Kuwe kuna Sheria kama hii ya kunisaidia mimi Wema niepukane na matusi Naona ni bora niendelee kutukanwa mpaka Siku nitakayokufa kuliko kuona fans wangu mimi, fans wa Wolper, fans wa Jokate, fans wa Ali Kiba, fans wa Diamond Platinumz na Wengine wengi wakinyang'anywa haki yao ya msingi kabisa ambayo ni haki ya kuweza kufungua mdomo na kuongea hata yale ambayo sisi mastar na wanasiasi hatukubaliano.....Je mimi kama Wema nitasemaje nawadhamini fans wangu ambao wao ndo wamenipa umaarufu huu na kunifikisha hapa nilipo kama hapo hapo nitawanyanyasa kwa kuwapokonya haki yao ya freedom of speech.

Mimi Wema sijakamilika , wote mnajua ninamapungufu yangu , je mimi Wema nitawezaje kujua makosa yangu ili niweze kubadilika na kufanyA vizuri kama sitokubali kusikiliza maoni ya watu wote yawe mabaya au mazuri?Nafikir wore mnajua hakuna page ya Mtanzania hapa instagram yenye matusi na malumbano kama page yangu mimi ....

Nimeshauriwa sana Kuwa nianze kublock wote wanaoniwekea comment za matusi na kufuta comments zao kama wanavyofanya mastaa wengine lakini nimegoma. Je mnadhani mimi nafurahia hizo comment za matusi? Tena Kwenye page yangu mwenyewe? Hapana zinaniumiza ila pia nakumbuka Kuwa mimi ni kioo cha Jamii nakumbuka Kuwa kabla ya Wema sepetu first comes nchi yangu .....

Niko tayari nitukanwe lakini haki za fans wangu, haters wangu na watanzania wote kwa ujumla ziwe po pale pale. Watanzania naomba tuungane katika kumsupport my dada Kwenye hili @iworeadress @iworeadress. Mimi nimemwelewa sana anachokisema. Tunaelekea pabaya Sasa....Tupiganie haki zetu za uhuru wa kuongea. Tusipojipigania hakuna wa kutupigania. Naamini Chama changu nachokipenda cha CCM kitatusikukiza wananchi wake na kufanyia hilo kazi.Tafadhali follow hii page ili tuweze kuchangia na kabadilishana mawazo . @ccmchangeorquit

0 comments:

Post a Comment