Pages

Subscribe:

Sunday, March 18, 2018

KITUO CHA RUNINGA CHA NCHINI MAREKANI BET CHAMPONGEZA DIAMOND PLATNUMZ


Kituo cha runinga cha kimataifa cha ‘BET ‘ kimetoa pongezi kwa msanii wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz baada ya album yake mpya ya ‘A Boy From Tandale’ kuingiza nyimbo tano zinazosikilizwa zaidi kwenye mtandao was iTunes nchini Burkina Faso.

Kituo hicho kimetoa pongezi hizo kupitia ukurasa wake wa Twitter kwa kuandika ”Hongera Diamond Platnumz kwa kuingiza nyimbo tano zinazosikilizwa zaidi...
nchini Burkina Faso kwenye mtandao wa iTunes”.

Jumatano Machi 14, 2018 Diamond Platnumz alizindua album yake ya ‘A BOY FROM TANDALE’ jijini Nairobi nchini Kenya.

0 comments:

Post a Comment