Pages

Subscribe:

Monday, March 12, 2018

MAVAZI YA WANAFUNZI WA SHULE YAMLIZA SNURA

Mavazi ya Wanafunzi wa Shule za Msingi Yamtoa Machozi Snuna
Staa wa miondoko ya mduara Bongo, Snura Mushi amefunguka kuwa amejikuta akizitolea macho sare za wanafunzi wa sekondari baada ya kuishia kuvaa za shule ya msingi kutokana na uwezo duni waliokuwa nao wazazi wake.

Snura au Mamaa Majanga aliliambia Ijumaa Wikienda kuwa, huwa anawaasa wasichana kwamba wamepata fursa ya kusoma, watumie nafasi hiyo kwa sababu yeye hakubahatika... kabisa kukanyaga sekondari wala kuvaa sare hizo, jambo ambalo linamfanya sasa hivi atumie nguvu ili wanaye wapate elimu.

“Kiukweli nikiona wasichana wamevaa sare za sekondari huwa ninazitolea macho sana. Natamani siku zirudi nyuma ili nami nipate elimu hiyo,” alisema Snura aliyeishia darasa la saba.

0 comments:

Post a Comment