Pages

Subscribe:

Monday, March 5, 2018

STORY YA DARASSA NA MADAWA YA KULEVYA IKIWA INAENDELEA BONGO DARASSA YUPO LASVEGAS KUPIGA SHOO

Mtayarishaji wa muziki nchini Tanzania, Abba amefunguka na kudai si kweli ukimya wa Darassa unatokana na matumizi ya dawa za kulevya kama baadhi ya watu wanavyodhani na kuwataka wawe wavumilivu kwani muhusika mwenyewe atakuja kujitokeza. 

Abba ametoa kauli alipokuwa anazungumza baada ya kuenea mfululizo wa tetesi zinazomuhusisha Darasa na matumizi ya dawa za kulevya na kupelekea...
kupotea katika tasnia ya muziki mpaka hii leo.

"Nashindwa kuwaelewa kwa jinsi mnavyosema Darasa haonekani sasa mmemuona vipi akiwa anatumia dawa za kulevya ?. Darasa yupo poa kabisa na labda hayo madude wanaosema wao wanayatumia wenyewe kwenye ndoto zao wanaoziota hao watu", amesema Abba.

Pamoja na hayo, Abba ameendelea kwa kusema "Darasa yupo poa na familia yake na wala hatumi kitu chochote mimi kama mwanae nasema yupo 'fresh' na kila siku nipo na Darasa na muda wote nikimuhitaji huwa nampata".

Kwa upande mwingine Abba na yeye anaonekana yupo sawa kwani ktk pita pita zangu huko insta nimekutana na post ya mwafrika aishie marekani na ni mwandaaji wa shows mbali mbali na amepost na kuipa promo show ya RayVanny na Harmonize huku pia akiwa ameandaa Show ya Msanii Darassa pia




BREAKING NEWS : BREAKING NEWS.
HARMONIZE Will be LIVE  in Las Vegas at The HARD ROCK CAFE during Rubgy Weekend,Performing all My Hits and New..Get your advance tickets at www.254lasvegas.com 
#WeGlobal🌍#MaPROMO #254Las



0 comments:

Post a Comment