Pages

Subscribe:

Sunday, March 4, 2018

WANACHAMA 48 WA KIKUNDI CHA WAKOREA WEUSI WAKAMATWA JIJINI MBEYA

Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Mbeya Mohammed Mpinga amesema wamekamata kundi la vijana 48 wanaodaiwa kufanya uhalifu mkoani Mbeya maarufu kama wakorea weusi  kwa tuhuma za kujihusisha na vitendo kupiga, kuua na kuibia watu vifaa mbalimbali wanaofahamika kama Wakorea.

Watuhumiwa hao wanadaiwa kufanya uhalifu huo wakitumia...
bisibisi, nyundo na tindo kuvunja nyumba na kuiba vitu kadhaa.

“Tumefanya Operesheni maalum pamoja na misako katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Mbeya. Operesheni hii ililenga kukamata wahalifu mbalimbali likiwemo kundi la vijana wanaojiita Wakorea ambao wamekuwa wakifanya vitendo vya uhalifu na kuhatarisha usalama wa raia na mali zao.” -Kamanda Mpinga

Kamanda  Mpinga amewaambia wanahabari  kuwa watuhumiwa hao bado wanaendelea kuhojiwa.
 

 

 


0 comments:

Post a Comment