Pages

Subscribe:

Tuesday, January 26, 2016

AY AFANYA RMX YA ZIGO ILI KUWAPA FUNZO WASANII WA NDANI

12509174_10153372908158379_166997376138407366_n

AY alisema kuwa amefanya Zigo rmx na Diamond ili kuwapa funzo wasanii wenzake wa ndani. Amesema kufanya remix ya wimbo huo na Diamond ni kuwaaminisha wasanii wa ndani kuwa wanaweza kufanya kolabo zao wenyewe kwa wenyewe na kwenda kimataifa.
 
“Dhana kubwa ya kufanya kazi na ‘artist’ mwenzangu wa nyumbani ni kuonesha kuwa tunaweza kutengeneza wimbo mkubwa na ukafanya vizuri Afrika nzima bila...
kutumia artist wa nje,” AY alikiambia kipindi cha XXL cha Clouds FM hivi karibuni.
“Hii itasaidia sana ‘kuchange mind’ za wasanii wenzangu. Haikatazwi au kupingwa kufanya na artists wa nje but ‘we wanna show them’ kuwa industry yetu imekuwa kubwa sana, so cha msingi tuunganishe nguvu pamoja,” alisisitiza.

Hadi sasa video ya wimbo huo imeangaliwa kwa zaidi ya mara 340,000 kwenye Youtube.

0 comments:

Post a Comment