Pages

Subscribe:

Tuesday, January 26, 2016

RAPPA KUTOKA TANZANIA ATAJWA KUWANIA TUZO ZA KORA NCHINI NAMIBIA

Rapper Wakazi kutoka hapa home Tz ambaye ni mkali kwenye anga za muziki wa Hip Hop ameingia kwenye Kinyang’anyiro cha kuwania tuzo “Kora_Awards ” ya Best Hip Hop Act 2016,  Tuzo ambazo zinategemea kutolewa...
March 20th huko Windhoek, Namibia.

Best Hip Hop Act 2016, Awards Nominees

Sarkodie (Ghana)
Stanley Enow (Cameron)
KO (South Africa)
Kiff No Beat (Ivory Coast)
Hamzaoui Med Amine (Tunisia)
Wakazi (Tanzania)

Hata hivyo kutoka Tanzania hatakuwa pekeyake bali, Vanessa Mdee, Diamond Platnumz, Yamoto Band na Mrisho Mpoto, pia ni wasanii ambao wanawania tuzo siku hiyo.
Kuhusiana na ushidi Rapper “Wakazi” amesema kuwa  “Kuwa nominated tayari kwangu ni ushindi tosha!! Nimekuwa nafanya Muziki officially kwa kama 4 years now na sijawahi kuwa nominated Tuzo yoyote ile hata mara Moja. So nomination hii ina maana kubwa sana kwangu na ukichukulia pia ni Tuzo Za kimataifa. Nikishinda nitafurahi ila haimaanishi kuwa nitakasirika nisiposhinda. Coz kuchaguliwa kwangu naweza kusema ni kutokana na ubora wa Kazi zangu, consistency Pamoja na support Ya mashabiki ambayo ndio iliyoweza kufanya nionekane.”
Hivyo kwa wadau wa muziki make sure that unaonesha support yako ya kutosha ili kuhakikisha  Rapper “Wakazi” anaibuka mshindi na kuipeperusha bendera ya Tanzania kupitia Muziki wetu wa Hip Hop. Umoja ni nguvu, Utengani ni udhaifu. Ili ashinde Please Send “Kora 123″ to +248984000 to vote for Wakazi (@Wakazimusic) as the #BestHipHopAct in 2016 @Kora_Awards.  Cheers 2016.

0 comments:

Post a Comment