Pages

Subscribe:

Monday, May 30, 2016

HASHEEM THABEET ATUA KIMYA KIMYA NCHINI TANZANIA

Tangu nimeanza kumsikia, Hasheem Thabeet hajawahi kuwa mtu wa matangazo mengi pale anaporudi nyumbani. Mchezaji huyo wa kikapu aliyefanikiwa kuchezea timu nne zilizopo kwenye ligi ya NBA nchini Marekani, yupo jijini Dar es Salaam kwa
Mchezaji huyo aliyeenda hewani, Jumamosi alionekana kwenye viwanja vya Leaders alikoenda kwenye tamasha la Nyama Choma.
Akiwa NBA Hasheem alichezea timu nne tofauti zikiwemo...
Memphis Grizzlies (2009 – 2011), Houston Rockets (2011–2012), Portland Trail Blazers (2012) na Oklahoma City Thunder (2012–2014).
Pia amechezea timu zingine za ligi ya chini, D-League Dakota Wizards, Rio Grande Valley Vipers na Grand Rapids Drive.

Katika misimu yote tisa aliyowahi kucheza, Hasheem alikuwa na wastani wa pointi 2.2, 2.7 rebounds, na 0.8 blocks kwa kila mchezo. Tafsiri yake ni kuwa mchezaji huyo hakuwa na mafanikio sana kwenye ligi hiyo.

0 comments:

Post a Comment