Pages

Subscribe:

Thursday, February 25, 2016

TEKNO AFUNGUKA UKWELI JUU YA MSICHANA KUTOKA TANZANIA GIGY MONEY

Kwa wale wanaofatilia stori za burudani Tanzania hasa ujio wa mwimbaji wa Nigeria Tekno kwenye show ya Dar es salaam walipata kilicho-trend kuhusu mwimbaji huyo staa wa hit single ya ‘wash‘ kuripotiwa kulala na Mrembo wa kitanzania aitwae Gigy Money.

Baada ya hizo taarifa kusambaa, Tekno alipost na kuandikiwa caption ya picha yake kwenye Instagram kwa Kiswahili akionekana kukasirishwa na kilichosambazwa na Mrembo huyu ambapo moja ya sentensi zilisomeka ‘umelala na... meneja wangu ukaletwa chumbani kwangu maana uliomba upige picha sasa unaleta stori kwamba umelala na mimi‘

Hii ishu ilimfanya Tekno aendelee kupokea maswali mengi ya media aliporudi Tanzania tena Waandishi wakimuuliza kuhusu Gigy huyohuyo… Tekno amesema hatopenda tena kuiongelea hii ishu wala kuulizwa ila akasisitiza...
‘Kabla ya yote sijui Gigy ni nani, ni mtu ambaye nilipiga nae picha tu, sina chochote cha kufanya naye… namuheshimu na wala sio namdharau ila ni kwamba simjui’

0 comments:

Post a Comment