Pages

Subscribe:

Wednesday, April 20, 2016

GIGY MONEY: MI MZUNGU NAMCHUKULIA NEY KAMA MWEHU

Mrembo anayefanya poa kwenye video za wasanii wa Bongo kama video model Gigy Money, amempa za uso msanii Ney wa Mitego na kumuita mpumbavu asiyejitambua ni nani, baada ya kumtapeli pesa yake. Gigy Money ameyasema hayo alipokuwa akiongea kwenye kipindi cha Planet Bongo kinachorushwa na East Africa Radio, na kusema kuwa kama msanii huwezi...
kuwaimba wenzako vibaya, huku ukiacha yale mabaya yako. 

“Ni upumbavu wake tu mi nilishamuonaga mwehu, kwa sababu kwa mtu ambaye anajua muziki huwezi ukaanza kuimba maisha ya wenzake wakati ya kwako yanakushinda”, alisema Gigy Money. Pia Gigy Money amesema pamoja na kumtapeli pesa hiyo ambayo alitakiwa kulipwa baada ya kuonekana kwenye video yake ya shika adabu yako, ameamua kumpotezea kwani hana shida ndogo ndogo, na pia ameamua kuwa na tabia ya kizungu, kutojali vitu ambavyo huenda vikaleta ugomvi kati yao. 

“Mi simaindi kwenye kuwekwa kwenye scene yeyote ya video as longer as nalipwa, lakini baadae tena anakuja kuniletea mambo ya kunipa hela ndogo, from laki tano to elfu 20 imagine, mi nimechukulia uzungu ningekuwa mswahili ningemdai dai, ningempigia simu, mi naendelea na maisha yangu ye atajua na maisha yake, sijawahi kumdai na wala simdai sina njaa hiyo ya hivyoo, naweza kuwa na laki tano ndani ya siku mbili au moja so what is laki tano, nigombane na watu tuwekeane mabeef kisa laki tano?”, alisema Gigy Money.

0 comments:

Post a Comment