Pages

Subscribe:

Tuesday, April 12, 2016

HUYU NDIYE NYOKA MKUBWA ZAIDI DUNIANI ALIYEKUTWA AMEKUFA

160411115054_giant_python_624x351_bbc_nocredit


Joka kubwa zaidi kuwahi kukamatwa duniani limekutwa likiwa limekufa.

Chatu huyo alipatikana katika eneo lililokuwa likijengwa nchini Malaysia karibu na mti mkubwa uliokatwa katika kisiwa cha Penang. Linakisiwa kuwa na urefu wa takriban na mita 8 hivi sawa na futi 26 lilipatikana...
siku ya Alhamisi iliyopita. Kwa bahati mbaya joka hilo lilikufa Jumapili lilipokuwa likizaa, afisa anayesimamia ujenzi katika kisiwa hicho cha Penang, Herme Herisyam aliiambia BBC.

160411115210_giant_python_624x351_bbc_nocredit


Kulingana na daftari za kumbukumbu za Guinness, joka anayeshikilia rekodi ya dunia anaurefu wa mita 7.67. Chatu huyo anayeitwa Medusa ana uzani wa kilo 158 na anaishi katika jumba moja mjini Kansas City, Missouri Marekani.

Hata hivyo joka huyo wa Malaysia ambaye alikuwa mkubwa zaidi yake hakuwa amepimwa na kuthibitishwa kuwa mrefu zaidi kabla ya kufa kwake.
Herisyan anasema kuwa alikuwa na uzani wa kilo 250.
Hata hivyo katika harakati za kumuokoa kutoka maficho yake inakisiwa kuwa aliumia na hivyo akafa kabla hajafikishwa kwenye hifadhi ya wanyama alikotarajiwa kutuzwa hadi ajifungue.

0 comments:

Post a Comment