Pages

Subscribe:

Monday, April 11, 2016

HAYA NDIYO MAISHA YA MBUNGE WA MBEYA MH SUGU

Kwenye Kampeni za uchaguzi Mkuu wa 2010 na 2015, Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi aka Sugu alijishusha na kujinyongesha ili wananchi wamwamini na kumpa kura. Miongoni mwa mambo aliyotumia kuombea kura ni kutomiliki Magari na Nyumba za Kifahari na badala yake atatumia fedha atakazopata kuwahudumia wananchi hasa kwenye huduma za Afya na Elimu. Moja ya ahadi kuu ya Mr Sugu ni hii hapa na nanukuu;

"Nikichaguliwa kuwa Mbunge, sioni faida ya kutembelea magari ya kifahari na kulala kwenye jumba la kifahari wakati...

wananchi wangu wanateseka kwa kukosa huduma bora hospitalini na watoto wanakosa vitabu, vyumba vya madarasa na madawati. Nitauza mpaka gari la Mkuu wa Mkoa ili kuhudumia Jamii========= Mwisho wa Kunukuu.

Sasa linganisha kauli hiyo na haya maisha anayoishi Mbunge wa Mbeya Mjini, Mr Sugu. Je kwa tafsiri yako msomaji, nini maana ya Magari ya Kifahari na Nyumba ya kifahari? Hivi anavyomiliki Sugu si vitu vya kifahari?

0 comments:

Post a Comment