Muigizaji wa Filamu Bongo, Shamsa Ford ameonekana kuvutiwa zaidi na sera ya Rais Dkt. John Magufuli ya kubana matumizi.
Kupitia mtandao wa instagram Shamsa ameeleza kuwa kutokana na
utaratibu huo wa Rais Dkt. Magufuli kila kijana kwa sasa anafanya kazi
kwani hapo awali wengi wao walipenda vya kupewa.
Tunalalamika maisha ni magumu sana labda kwakuwa
hatujazoea hii hali..Ila mm nakupongeza sana raisi wangu kwa kazi
unayoifanya. kwanza umetusaidia...
vijana kuwa wabunifu kila siku.
Tulikuwa
tumezoea kupewa tu na kazi hatufanyi ila kwa sasa naona kila kijana
anafanya kazi kwa bidii na kuheshimu pesa vizuri.Hii itasaidia hata kwa
uchumi wa nchi kukua kutokana na kwamba kila kijana anafanya kazi kwa
bidii..Mungu akubariki sana Raisi wangu na azidi kukulinda kwa kila
mwenye nia mbaya na wewe #UZALENDOKWANZA#
Katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 ambao ulimuweka madarakani Rais
Dkt. Magufuli, Shamsa alikuwa akimpigia debe Edward Lowassa ambaye
alikuwa akiungwa mkono na vyama vinavyounda Ukawa.
Tuesday, August 15, 2017
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment