Pages

Subscribe:

Sunday, August 27, 2017

WIMBO MPYA WA ALIKIBA SEDUCE ME WAWEKA REKODI MPYA AFRIKA MASHARIKI

Msanii wa muziki wa bongo fleva Alikiba ambaye amepewa cheo cha 'Mfalme' na mashabiki wake, amedhihirisha kuwa mashabiki hawakukosea kumpa cheo hicho, kwa kuvunja rekodi ya kutazamwa kwa video yake kwa mara nyingi zaidi ndani ya muda mfupi.

Kwenye ukurasa wake wa instagram, Alikiba ambaye siku ya Ijumaa ameachia video ya wimbo mpya ya 'Seduce me', ameweka...
post akiwashukuru mashabiki wake kwa kufanikisha kuvunja rekodi hiyo.

"Ahsanteni sana kwa upendo, nisingebarikiwa zaidi na kupendelewa bila nyinyi, nyinyi ni wa maana sana kwangu na nafanya haya kwa ajili yenu", aliandika Alikiba.

Pamoja na hayo kwenye ukurasa wa instagram wa kampuni kubwa inayosimamia muziki wa Alikiba ya Rockstar. imeandika kuhusu rekodi ya video hiyo ambayo bado inaendelea kushika namba moja kweny video zinazotrend.

Historia ya kunjwa rekodi imewekwa, Mfalme Kiba na wimbo wake mpya wa 'Seduce me' umekuwa wa kwanza na kipee kwa msanii wa Afrika Mashariki kufikia kutazamwa mara milioni 1 kwenye Vevo/YouTube ndani ya masaa 38 tu, ina 'trend'namba 1 Tanzania na namba 1 Kenya kwa 'weekend' nzima, rekodi imevunjwa”, iliandika Rockstar.
 

0 comments:

Post a Comment