Pages

Subscribe:

Sunday, June 19, 2016

RAMA D AFUNGUKA KUHUSU YEYE NA JIDE

Mwanamuziki wa R&B nchini Tanzania Rama D, amekanusha vikali habari zilizotapakaa mtandaoni kwamba kwa sasa anatoka kimapenzi na mwanadada Lady Jay Dee, amesema wanaheshimiana sana na haiwezi kutokea kitu kama hicho daima.

Hata hivyo Rama D ameendelea kusema kwamba yeye anamfaham mpaka mpenzi wa mwanadada Lady Jay Dee na kusema hata siku ya show ya ‘Naamka Tena Concert’ alipanda...
jukwaani kuonesha jinsi anavyomkubali mwana dada huyo.

Rama D anasema anawashangaa sana watu wanaoenda kufanya video zao nje na kusema kwamba haoni sababu ya kufanya video hizo nje kwani hapa nyumbani kuna mazingira ya kutosha kufanya video nzuri zitakazoitangaza nchi.

0 comments:

Post a Comment