Pages

Subscribe:

Wednesday, August 9, 2017

CJAMOKER AFUNGUKA ALIVYO TAKA KUJIUA WAKATI YUPO ICU

Msanii na mtayarishaji wa muziki wa bongo fleva ambaye pia ni mmoja wa wasanii wanaounda kundi la SSK, Cjamoker amesema ilibakia kidogo ajitoe uhai wake kipindi alipokuwa amelazwa katika chumba maalum cha wagonjwa mahututi ICU. 

Cjamoker amebainisha hayo leo wakati alipokuwa anazungumza baada ya kuulizwa swali na mmoja wa waongozaji kuhusiana na maisha yake aliyoyapitia katika...
kuumwa.

"Nilitaka kujiua nilipokuwa ICU, maana kuna siku nilikuwa naota ndoto kama hospitali imevamiwa na madudu halafu yakawa yanauwa 'Nurse' sasa mimi kwa kutaka kujiokoa nikajikuta najitoa mipira niliyokuwa nimewekewa kunisaidia kupumua na kusababisha hali ya taharuki kwa madaktari pindi walipokuja, kwani madaktari hao baadhi yao walikuwa hawawezi namna ya kuirudisha mipira hiyo hivyo ilibidi waniwekee dripu la kawaida mpaka asubuhi ndipo nilipokuja kuwekewa mipira hiyo na madaktari wengine", amesema Cjamoker.

Pamoja na hayo, Cjamoker ameweka wazi jambo ambalo lilimpelekea kuumwa kwa kipindi kirefu na kushindwa kufanya kazi ya aina yoyote ile na mwisho kuwa mtu wa kulala tu.

“Kitu kilichokuja kunisababishia mimi kuumwa ni kutokula kwa wakati, nilikuwa napitiliza kutokula kwa wakati, unajua kazi zangu ni production nakuwa busy, wakaniambia utumbo umetoboka, umejikunja na pia waligundua na henia, pia wakaniambia matumizi ya pombe ingawa nilikuwa situmii sana”, alisema Cjamoker.

Kwa upande mwingine, Cjamoker amesema anawashukuru wazazi wake kwa upendo waliyokuwa wamemuonyesha wakati alipokuwa yupo kitandani kwa maana kuna vitu vingine alikuwa hawezi kuvifanya yeye kama yeye.

0 comments:

Post a Comment