Msanii wa Hip hop anayewakilisha Kanda ya Kati, Moni Cetrozone
amewataka mashabiki zake kutomfikiria yeye kuja kuimba siasa kutokana na
matatizo ya utekwaji aliyoyapata Aprili 05, 2017 akiwa na Msanii Roma
Mkatoliki.
Moni amefunguka na kusema atashangaa sana kuona
kama kuna shabiki anayesubiri yeye aimbe nyimbo za kuhusu...
tukio la
kutekwa kwani ni kitendo ambacho hajawahi kukifanya tangu anaanza
kufanya muziki.
"Mimi nyimbo zangu nyingi
zinahusisha maisha niliyoshi huko Majengo Sokoni, changamoto za maisha
ya watu wangu wanazopitia pamoja na yale niliyoishi. Hata ukisikiliza
wimbo nilioshirikiana na Roma nimeimba maisha na siyo siasa. Mashabiki
wasidhanie kwamba nitaimba matukio yale lakini nachotaka tu kuwaambia
wakikusanya nyimbo zangu zote wanaweza kutengeneza albamu" Moni
Kuhusiana na kumshirikisha baraka katika
wimbo wake mpya Moni amesema ni suala la kibiashara ndilo alilozingatia
haswa kwa msanii kama Baraka The Prince ambaye tayari ana mashabiki wa
kutosha.
"Naamini sana kolabo kwani
hata kolabo ya Roma 'Usimsahau mchizi ni wimbo ulioniweka kwenye nafasi
nzuri hivyo hata hii ya Baraka najua utanifikisha sehemu nzuri zaidi" - alisisitiza Moni



Follow on Instagram
0 comments:
Post a Comment