Pages

Subscribe:

Friday, April 24, 2015

TAJIRI NAMBA MOJA AFRICA DANGOTE ATEMBELEA UFUKWE ATAKAO JENGA BANDARI YAKE HUKO MTWARA

Biionea Alhaji Aliko Dangote amekabidhiwa hekari 2,500, katika halmashauri ya Wilaya ya Mtwara ili ajenge bandari itakayotumika kusafirisha saruji kutoka kiwandani hapo kwenda... maeneo mbalimbali ya ndani na nje ya nchi.


Mfanyabiashara maarufu Afrika, ambaye ni Mwenyekiti na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Viwanda vya Dangote Group of Industries, Alhaji Aliko Dabgote akinyoosha mkono kuangalia eneo la ufukwe wa Bahari ya Hindi katika Kijiji cha Mgao, Kata ya Maumbu, Tarafa ya Mayanga, Mtwara Vijijini, ambapo atajenga bandari yake ya kisasa kwa ajili kusafirisha saruji itakayozalishwa kwenye kiwanda chake kikubwa kinachojengwa katika Kijiji cha Msijute.
Alhaji Dangote akishuka kwenye ndege na kulakiwa na Mwakilishi Mkazi wake hapa nchini, Esther Baruti

Mwenyekiti wa Kijiji cha Mgao, Shaa (kushoto) akimuonesha Dangote eneo la uwanja aliopewa na wanakijiji kwa ajili ya ujenzi wa mkazi yake. Kijiji nacho kitanufaika na Dangote ambaye atawajengea shule, hospitali pamoja na miradi mingine ya maendeleo


Msafara wa Dangote ukitumia magari kutembelea kiwanda cha saruji kinachojengwa

0 comments:

Post a Comment