Pages

Subscribe:

Wednesday, June 24, 2015

AUNT EZEKIEL: SIPENDI MWANANGU AWE MWIGIZAJI

Aunty Ezekiel: Sipendi Mwanangu Awe Mwigizaji
Staa wa Bongo Movie,Aunty Ezekiel amefunguka kuwa hapendi mtoto wake aliyejifungua hivi karibuni aitwaye Cookie,awe mwigizaji wa filamu kama yeye.
Akizungumza na Clouds Fm, alisema kuwa atakachofanya kama mzazi anataka mtoto wake asome na kama...
akiwa mwigizaji basi iwe kama kazi yake ya ziada siyo anayoitegemea kwenye maisha yake.
‘’Binafsi sipendi mwanangu awe mwigizaji kama mimi,na siyo lazima kama mimi mama yake niwe mwigizaji na yeye awe hivyo kuna kazi nyingi ila ninachotaka asome sana na kama atataka kuwa msanii basi iwe kazi yake ya pili siyo aitegeeme katika maisha yake,’alisema Aunty.
‘’Hata mimi pamoja na kwamba ni mwigizaji lakini siitegemei sana kazi hiyo nina kazi zingine nafanya,’’aliongezea Aunty.

0 comments:

Post a Comment