Pages

Subscribe:

Friday, September 18, 2015

NAY WA MITEGO AWEKA WAZI UHUSIANO WAKE NA PAM DAFF

 Msanii Ney wa mitego amefunguka juu ya taarifa zilizoenea kwenye mitandao ya kijamii kwamba ana mahusiano ya kimapenzi na Msanii wa Bongo Flava mwenye figure matata Pam Dafa, na kusema wao ni...
marafiki tu.
"Mi na Pam D ni washkaji, na siwezi nikasema tuna mahusiano ya hivyo japokuwa watu wanahisi kama tuna mahusiano ya hivyo, Pam D ni mshkaji wangu alafu mshakji wangu long time kabla hajawa serious na maswala ya muziki, ndio maana tupo karibu hivyo", alisema Ney alipokuwa akiongea kwenye kipindi cha Planet Bongo kinachorushwa na East Africa Radio.
Ney wa mitego aliendelea kufunguka na kusema kwamba situation ambazo zipo kwa vijana zingine zinatokeaga tu kama bahati mbaya.
"Unajua ngoja nikwambie tu sometimes tunabakia kuongea tu situationa au hali ambayo ipo kwa vijana ambao tunaishi leo, kuna vingine vinatokeaga tu kama bahati mbaya na huwa vinatokeaga kwamba bwana ehee hatuwezi kuwa permanent, huwa zinatokeaga, mi Pam D mshkaji wangu tu", alisema True boy Ney wa mitego.
Team ya Planet bongo haikuishia hapo, iliamua kumtafuta Pam D na kupata upande wa pili wa maelezo nae akajibu haya " sio kila kitu mpaka ukiweke wazi, inawezekana ni kweli lakini huwezi jua kama je itafikia hatua hiyo, watu wanaogopa labda unajua ukiweka vitu nje mwisho wa siku mambo yanakuja kuharibika", alisema Pam D.

0 comments:

Post a Comment