Pages

Subscribe:

Wednesday, October 21, 2015

BARAKAH DA PRINCE KUJENGA MAKTABA KWENYE ALIYO SOMA


Braka da Prince ameeleza mpango wake wa kujanga maktaba ya shule ya msingi aliyowahi kuisomea kama kurudisha shukrani kwa jamii .
Akiongea na Planet Bongo ya East Africa Radio, muimbaji wa ‘Nivumilie’ amesema kuwa  ameamua kufanya hivyo ili kurudisha fadhila kwa jamii anayotoka baada ya kupata mafanikio kupitia...
kipaji chake cha kuimba muziki.
“Unajua mi sio mtu ambaye nafanyaga vitu but sio mtu ambaye naongea na kuzungumza sana labda kama nimefanya nini, kwa hiyo na shule ambayo mi nimesomea inaitwa Pamba primary school kuna kitu ambacho nataka nifanye, nataka nikatengeneze maabara ya vitabu kama Mungu akisaidia”, alisema Baraka.
Licha ya kujenga maktaba shuleni hapo, Baraka anatarajia kugawa vitabu, madaftari na vifaa vingine kwa wanafunzi wanaosoma shuleni hapo.

0 comments:

Post a Comment