Pages

Subscribe:

Friday, March 11, 2016

BOB JUNIOR AKAMATWA KWA TUHUMA ZA KUSHIRIKIANA NA MAJAMBAZI

Msanii wa muziki wa bongo fleva Bob Junior amekamatwa na jeshi la Polisi nyumbani kwao magomeni mapipa Jijni Dar es salaam majira ya saa sita mchana wa leo. Kwa mujibu wa chanzo cha  habari ambaye ni rafiki wa karibu wa Bob Junior ameiambia Mtembezi.com kuwa Polisi wamemkamata Msanii huyo kwa kile walichodai kuwa wamepata taarifa kuwa Bob Junior anashirikiana na kikundi cha...
majambazi.

Rafiki huyo wa karibu na Bob Junior, ameiujuza mtembezi.com kuwa Msanii huyo amekuwa akipigiwa simu tangu juzi kutoka kituo cha polisi cha magomeni usalama kwamba kuna lalamiko la mtu anaye dai kutekwa na kikundi cha majambazi ambacho msanii huyo anashirikiana nacho.

0 comments:

Post a Comment