Pages

Subscribe:

Saturday, March 26, 2016

Listen & Download: SAUTI YA JACK CLIFF AKIZUNGUMZA KUTOKA NDANI YA GEREZA NCHINI CHINA

Mtanzania aliyefungwa gerezani China, ampigia simu Millard Ayo akiwa ndani ya gereza na kuelezea namna alivyokamatwa kwa ishu za dawa za kulevya, maisha wanayoishi gerezani na Idadi ya Watanzania waliofungwa huko.


Play Here


Katika exclusive interview Mtanzania huyu anasema ‘Ilikuwa mambo ya madawa, mimi nilikuwa nimetoka Dubai kuja China, jamaa wakaingia katika hoteli na wakatukamata, jumla tulikuwa watu nane‘

‘Ujue nchi hii mambo ya madawa wanapiga vita mno, kesi ya madawa zina adhabu ya miaka mingi kuliko kesi nyingine yoyote, kama mimi nimepewa miaka kumi na miezi sita‘

‘Mimi nimefungwa nikiwa na miaka kama 26, nilianza kufanya biashara ya dawa za kulevya nikiwa na miaka kama 18, hawa jamaa wa China ni wabaguzi sana, hivyo unatakiwa uwe kauzu ili kuendana nao sawa‘

0 comments:

Post a Comment