Pages

Subscribe:

Thursday, March 17, 2016

VIATU VYAMFANYA KANYE WEST APIGE PICHA NA DIAMOND

Muziki wa Bongo Fleva umeanza kulipa, tunaweza tukawa nchi ya tatu Afrika baada ya Nigeria, Afrika Kusini. Hivi karibuni picha kibao zilisambaa mitandaoni baada ya msanii, Diamond Platnumz kupost picha akiwa na staa wa Hip Hop kutoka nchini Marekani, Kanye West. Diamond amesema ‘Kanye West alivutiwa na viatu vyangu ambavyo nilikuwa nimevivaa.’

Akizungumza kwenye kipindi cha Planet Bongo, kinachoruka kupitia EA Radio, Diamond alisema,
“Nilipokuwa airport pale Los Angeles tunasubiri kuchukua mabegi yetu, nilisikia mtu akisema ninaweza... kupiga picha viatu vyako? Kwakuwa alikuwa ameinama sikuweza kumtambua lakini alipoinuka nikashangaa kumuona ni brother Kanye West. Nilimuomba tupige picha kwanza halafu vingine vitaendelea.”

“Tumuombe Mungu mambo yaendelee vizuri kama tulivyopanga, kuna kitu kizuri kinaweza kikatokea kati yetu,” aliongeza Diamond.

0 comments:

Post a Comment