Pages

Subscribe:

Friday, November 24, 2017

ENOCK BELLA: MUNGU KAMJAALIA ASLAY KIPAJI NA MTUNZI MZURI



Kwa namna msanii Aslay anavyoachia ngoma kila wakati, mashabiki wamekuwa wakitania huenda aliondoka na daftari la nyimbo katika kundi la Yamoto Band, sasa Enock Bella amejibu kuhusu hilo.

Muimbaji huyo wa ngoma ‘Sauda’ amesema hapana hilo halipo ni Mwenyenzi Mungu tu kamjalia Aslay kipaji na mtunzi mzuri kitu ambacho hata yeye...
anakipenda.

“Unajua yote hiyo kwa sababu hakutaka promo kuwa kigezo chake kikubwa sana kwa hiyo akatumia kwa  kuwepo nafasi hii anaweza akafanya vitu vingi sana, kwa hiyo anafanya kile kitu alichonacho” Bella ameiambia E Fm.

Tangu kusambaratika kwa kundi la Yamoto Band Aslay ametoa ngoma nyingin zaidi ukilinganisha na wasanii wenzake waliokuwa wakiunda kundi hilo (Bella, Beka na Maromboso).

0 comments:

Post a Comment