Pages

Subscribe:

Sunday, January 28, 2018

AKOTHEE: NALIPWA KUTEMBEA UTUPU



Muimbaji Akothee kutoka nchini Kenya ambaye wengi tulimfahamu baada ya kumshirikisha staa wa Bongofleva Diamond Platnumz kwenye wimbo wake wa Sweet Love, leo ameingia kwenye headlines Kenya baada ya watu kukosoa tabia yake ya kupost picha katika mitandao ya kijamii zikionyesha maungo yake.

Akothee amezichukua headlines baada ya kuamua kuwajibu wale wanaomkosoa kuwa anavaa nguo za nusu uchi, kitu ambacho hawakipendi na sio vizuri kwake kwani yeye...
hapaswi kufanya hivyo kutokana na kuwa mama watoto watano.

Baada ya stori hizo kuenea na kuonekana Akothee zimemfikia alitumia ukurasa wake wa instagram kuwajibu wanaomsema na kumuandama , Akothee ameandika hivi “I get paid to walk naked get your beach accessories @garodaboutique order your suncream and let your skin glow like #MadamBoss @garodaresortkenya”

Tafrisi ya maneno ya Akothee ni “Nalipwa kutembea utupu pata nguo zako za beach kwa @garodaboutique oda SunCream ili ngozi yako iwe nzuri kama #MadamBoss @garodaresortkenya” Sun Cream ni mafuta ya ngozi kwa ajili ya kuzuia ngozi isiharibiwe na mionzi ya jua.

0 comments:

Post a Comment