Pages

Subscribe:

Friday, January 26, 2018

DONALD TRUMP APEWA CHOO CHA DHAHABU BADALA YA PICHA YA VAN GOGH

Choo cha dhahabu alichopendekezewa rais Donald Trump
Jumba la kumbukumbu la Guggenheim mjini New York limekataa ombi kutoka kwa rais Donald Trump la kutaka kupewa mchoro wa msanii Van Gogh ili kuwekwa katika ikulu ya Whitehouse kulingana na vyombo vya habari.

Jumba hilo liliomba msamaha kwa kutoweza kupeana picha hiyo na badala yake likaomba kumpatia rais Trump choo cha dhahabu kulingana na...
gazeti la The Washington Post.

Lakini jumba hilo la kumbukumbu lilipendekeza limpatie rais Trump kiti hicho cha choo chenye dhahabu karati 18.

Ikulu ya Whitehouse haijatoa tamko lolote.

Kulingana na gazeti hilo,mhifadhi wa vitu katika jumba hiloi Nancy Spector aliojibu ombi hilo la Ikulu mwezi Septemba.

''Naomba msamaha...kukujulisha kwamba hatuwezi kushiriki katika kukupatia picha hiyo kwa kuwa ni miongoni mwa mkusanyiko wa Thannhauser ambao hawaruhusiwi kutoka nje ijapokuwa kwa maswala yasio ya kawaida'', aliandika katika barua pepe.

Picha hiyo ya 1888 ya Van Gogh, barua hiyo iliongezea itaonyeshwa katika taasisi dada kutokana na ruhusa kutoka kwa wamiliki wake. 

Hatahivyo , muhifadhi huyo ameongezea kwamba choo hicho cha dhahabu kilichotengezwa na msaani wa Itali Maurizio Cattelan kiko tayari kwenda Ikulu kwa ''mkopo wa muda mrefu''.

Ni jambo la kawaida kwa marais wa Marekani na wake zao kuomba kazi za usanii ili kupamba baadhi ya vyumba katika Ikulu ya Whitehouse.

0 comments:

Post a Comment