Pages

Subscribe:

Tuesday, September 26, 2017

NIKKI WA PILI AFUNGUKA SABABU ZA WEUSI KUTO SAINI WASANII


Msanii wa muziki wa hip hop Bongo kutoka kundi la Weusi, Nikki wa Pili amefunguka sababu za wao kutosaini wasanii. Rapper huyo ambaye kwa sasa anafanya vizuri na ngoma yake mpya ‘Kihasara’ amedai kuwa kuamua kumsaini msanii ni kukubali kubeba ndoto zake zote alizonazo kitu ambacho kwa sasa hawapo tayari.

“Ukisema unafungua label au una kumsaiini mtu, ina maana anakukabidhi ndoto zake mikononi mwako, je unaweza kuzifikisha??, watu wanataka...
watengeneza maisha yao, sisi tunavyoona bado,” amesema Nikki wa Pili.

“Unamuona Chin Bees tumekuwa naye kitambo kwanini hatukumsaini lakini tumemsaidia mpaka amekuja kupata Wanene. Nikisema sasa hivi namsaini Chin Bees atanidai video kama tatu, atanidai promotion, hiyo itakuwa baadaye one step at a time,” ameongeza.

Nikki wa Pili ameshafanya kolabo tatu na Chin Bees ya kwanza ikiwa ni Role Model, Sweet Mangi na sasa Kihasara

0 comments:

Post a Comment