Pages

Subscribe:

Saturday, September 30, 2017

SHOLO MWAMBA ATOBOA SIRI YA UGOMVI WA DOGO JANJA NA YOUNG D CHANZO NI MUNA

Msanii wa Singeli bongo Sholo Mwamba ametoa siri ambayo wengi walikuwa hawafahamu juu ya ugomvi wa Young Dee na Dogo Janja na kusema Muna love ndio chanzo cha bifu hilo kubwa kwa sasa. 

Sholo Mwamba amesema alishawahi kuwakuta wasanii hao na bosi wake 'Muna Love' wakijiachia na...
kueleza kwamba 'Madogo' hao wanagombania penzi la Muna love.

"Wahuni hawa nimeyasikia mazingira yao sema wanayumba kimazingira fulani, habari zao miyayusho, tena ving'asti tu wanajisahau, si wenyewe tunawakuta kwa bi mkubwa wamekaa miguu juu, mambo yao yametokea wanagombania mademu, baada wafanye muziki wao wanafelisha michongo, sababu zao wanagombania bi mkubwa wanafugwa fugwa tu na bi mkubwa", amesema Sholo Mwamba.

Sholo Mwamba ameendelea wa kusema kwamba pamoja na kwamba ameshagombana na bosi wake huyo lakini hakuweza kumuita Young Dee au Dogo Janja baba, kwani ni jambo ambalo halimuingii akilini.

"Mimi siwezi kumuita Dogo Janja baba, siwezi kumuita Young Dee baba, hata ukiangalia ugomvi wao sababu ni demu na demu mwenyewe ni bosi wangu", amesema Sholo Mwamba.

Young Dee na Dogo Janja sasa hivi wamekuwa paka na panya, huku wakitishiana usalama kila mmoja kwa kutaka kumpiga mwenzake akimuona.

0 comments:

Post a Comment